SSA | Hero-L | VI24 | Breeding for Africa

Uhamili kwa ajili ya Afrika

Rijk Zwaan iko Afrika kote. Ili kuendeleza uwezo halisi wa bara hili muhimu, tuna mtazamo wa muda mrefu. Tumewekeza kwenye kituo cha uhamili na kwa makusudi kabisa tumechagua kuendeleza aina chotara tu.

Lengo

Kilimo cha mazao chotara kinahitaji umakini mkubwa wa wakulima katika uwekezaji,  lakini kina faida kubwa kutokana na mazao mengi na bora zaidi.  Ili kuisaidia sekta ya mboga barani Afrika ikuwe kunahitajika  aina bora (za mboga), utaalamu mzuri na subira nyingi. Hii itawapa wakulima wadogo  nafasi muhimu katika ujenzi wa chanzo endelevu cha chakula barani Afrika. Lengo letu ni kusaidia katika ukuaji wa ongezeko la upatikanaji wa mboga zenye lishe na kuwasaidia wakulima wa Afrika kuinua kipato chao.

Rijk Zwaan Afrisem

Katika kituo chetu cha uzalishaji cha Rijk Zwaan Afrisem huko Arusha, Tanzania, tunahamili mboga chotara za kiafrika: ngogwe, sukuma wiki na pilipili mbuzi. Tunahamili pia nyanya fupi. Vile vile, aina nyingine za mboga kutoka mabara mengine zinatathminiwa ili kubaini uwezo wake wa kulimwa katika maeneo ya Afrika Mashariki na Afrika Magharibi. Tumeajiri wafanyakazi 70 na tuna hekta 20 za ardhi ya kilimo, ikijumuisha mashamba ya majaribio, mabanda ya kulimia (greenhouses) na vitalu vya kutenga (isolation blocks) vyenye viwango vya kisasa vya Rijk Zwaan. Shamba letu la maonyesho linatuwezesha kuonyesha na kutathmini wigo wetu (wa mazao) na mbinu zetu za kilimo mwaka mzima.

Mtazamo wa kibiashara

Mbegu zetu barani Afrika huuzwa kupitia kampuni zetu tanzu za mauzo (huko Afrika Kusini, Moroko, Misri na Tanzania) na mtandao mkubwa wa wasambazaji na wasimamizi wa mauzo. Katika maeneo mengi wakulima bado wako katika kujifunza mbinu bora za kulimo cha mboga. Ndiyo maana tuna timu maalum ya washauri wa kilimo wenye uzoefu inayolenga kuwajengea uwezo huo. Kwa vile wako katika kitovu cha soko husika (washauri hao) wanaweza kutoa ushauri wa kitaalamu unaoendana na hali halisi.

Kusambaza maarifa ya kiufundi

Wakulima wa Afrika wana mahitaji mengi zaidi ya aina bora za mboga.  Kiukweli, aina bora ni mwanzo tu kwa vile kuna vitu vingi vya kuendeleza katika kuboresha taaluma na mbinu za mauzo. Kwa vile tunahitaji wingi na uwepo wa wataalamu katika eneo husika ili kuongeza mafanikio, tunajitahidi kujenga ushirikiano na asasi za kiserikali, vyama vya wakulima na taasisi za mafunzo barani kote. Tunafurahi tunapochangia ujuzi wetu na utaalam katika miradi ya muda mrefu kama vile AIMSEVIAHorti-Impact na Smart.

Kuendeleza soko pamoja

Bado kuna mambo mengi ya kuendeleza katika kilimo cha bustani barani Afrika katika nyanja za mbinu za ugavi (logistics), usimamizi wa fedha, ubora, masoko na ujasiriamali. Kwa kuwa karibu na mkulima tunataka kuwapa uzoefu wetu na kubadilishana mawazo na serikali, wagavi wa mboga, taasisi za mikopo midogo na wadau wengine. Kama moja ya shughuli zetu tunajaribu kuwaunganisha wakulima na mabenki, wagavi na taasisi za masoko ili waweze kuendesha biashara zao kwa utaalam zaidi. Hatimaye jamii zao pia zitanufaika kwa kukuwa kwa uchumi.

Kuhamasisha ulaji wa mboga

Ulaji wa mboga ndiyo njia endelevu zaidi ya kupambana na ukosefu wa virutubisho. Ili kuhamasisha ulaji wa mboga barani Afrika, tunatambua kwamba ni muhimu kuwa na aina za mboga za jadi zinazohimili hali ya hewa ya pale. Kwa hiyo, tunatumia vianzilishi (vya mimea) kutoka katika taasisi kama vile Kituo cha Mboga cha Kimataifa (World Vegetable Center). Vile vile tunajiunga na miradi kama vile Amsterdam Initiative against Malnutrition (AIM) ambayo inaunganisha wadau mbalimbali ili kuimarisha usalama wa chakula na lishe kupitia wigo mpana wa miradi.  


People at the center

Kujituma

Tanzania ina nafasi maalum mioyoni mwetu. Hii ilianza mwaka 2002 tulipoanza kuzalisha mbegu pale Arusha. Tulichagua eneo hilo kwa sababu ya hali yake nzuri ya hewa kwa uzalishaji wa mbegu za ubora wa juu.
undefined

Kutoa mbegu mpya chotara ni jambo la kuridhisha sana

Bertha Beganyi ameifanyia kazi Rijk Zwaan tangu 2014. Jukumu lake ni kuchagua pilipili kali. Anaweza kutumia jukumu hili kuendelea kutoa mbegu mpya, hivyo kulisisimua soko – na wakati mwingine hata kujisisimua mwenyewe.
undefined

Kuona ni kuamini

Robert Tiemtoré hufanya kazi ya ukuzaji wa bidhaa kwa niaba ya Rijk Zwaan nchini Burkina Faso. Hapa, watu wanapenda mboga sana, lakini viwango vya utaalam wa kiufundi wa wakulima viko chini sana. Mbinu ya asili inahitajika ili kuboresha hali hii. Ukiachilia mbali kuchagua aina ya asili humu nchini, changamoto kuu ni kufikia idadi kubwa ya wakulima wadogo wadogo.
undefined

Pamoja tunajaribu kuziba pengo la maarifa

Elijah Mwashayenyi ni mkurugenzi mtendaji wa SEVIA, taasisi ya ushirikiano wa sekta ya umma na binafsi inayolenga kuendeleza biashara ya mboga barani Afrika kwa kuingiza teknolojia na aina za mboga chotara na pia kuwaongezea wakulima maarifa ya kiufundi.
undefined

Huu ndiyo muda muafaka wa kuwekeza

Jacqueline Mkindi ni Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Kilimo cha Bustani cha Tanzania, ambacho huwakilisha wakulima 25,000 kote nchini. Lengo lake ni kukuza na kuendeleza sekta ya kilimo cha bustani.
undefined

Benki ya vinasaba isiwe makumbusho

Marco Wepereis (katikati kwenye picha) ni Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Kimataifa cha Mboga (World Vegetable Centre – WorldVeg), taasisi isiyo ya kifaida ya kimataifa ya tafiti na maboresho mahsusi kwa ajili ya mboga. Anakubaliana na mtazamo wa Rijk Zwaan kwamba mboga zina nafasi muhimu katika maendeleo ya Afrika.